Nyota wa Barcelona raia wa Uturuki, Arda Turan ameomba shinikizo lake la kuondoka klabuni hapo liweze kufanyiwa kazi ili aachane na klabu hiyo, mwenyewe akidai amechoka kukaa benchi.
Turan alisema "ni kweli Barcelona ni moja ya klabu kubwa duniani, lakini kwangu naona muda umefika kuondoka hapa kwenda kutafuta changamoto sehemu nyengine"
Turan aliyesajiliwa akitokea Atletico Madrid amekuwa na wakati mgumu klabuni hapo akishindwa kutoboa na kuingia katika kikosi cha kwanza.
Post a Comment
Post a Comment