Kambi za wakimbizi wa Burundi nchini Tanzania, zinakaribia kuzidiwa na uwezo wa kuwapa hifadhi maelfu ya wakimbizi wanaoendelea kuingia nchini humo karibu kila siku.
Shirika la Kimataifa la Madktari wasiokuwa na mipaka la MSF linasema hali hii ni hatari na huenda hali ikawa mbaya zaidi ikiwa hatua za dharura hazitachukuliwa.
MSF inasema kati ya wakimbizi Laki tatu waliokimbia Burundi, zaidi ya laki mbili wanaishi nchini Tanzania katika kambi ya Nyarugusu.
Idadi hii ya wakimbizi waliofurika katika kambi hiyo inatishia kulipuka kwa magonjwa kama kipindupindu kutokana na maji safi ya kunywa, ukosefu wa chakula na hata maswala ya usalama.
Post a Comment
Post a Comment